Mkurugenzi wa Operesheni ya Takwimu Bi, Radegunda
Maro (kulia) akiongea na wamiliki mbalimbali wa vyombo vya habari nchini juu
ya namna ya Uelimishaji jamii kwenye Sensa inayotarajia kuanza mapema mwezi
ujao tarehe 26 ambapo alisema kuwa wao kama tume nzima wamejipanga sawasawa
katika uelimishaji wa jamii juu ya swala hilo la sensa. Mkutano huo umefanyika
leo katika Hoteli ya PeakCook jijini Dar es Salaam.
Kamishna wa Sensa nchini Bi, Hajjat Amina Mrisho
(kushoto) akielezea namna walivyojipanga kushirikiana na vyombo vya habari
katika mkutano huo ambapo alisema kuwa wametenga kiasi cha Bilioni 141.5 kwa
ajili ya kuhakikisha kuwa swala hilo linakamilika ipasavyo. kulia ni Mkurugenzi
wa operesheni ya Takwimu Bi, Radegunda Maro.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya The Guardian Bw,
Kiondo Mshana wa kwanza kushoto pamoja na wakurugenzi wengine wakisikiliza kwa
makini mjadala huo.
Mwandishi wa habari kutoka wapo Radio Bw, Willison
Kibubu akiuliza swali kwenye mkutano huo.
OFISI
ya Taifa ya Takwimu (NBS), imetangaza kutoa matokeo ya sensa ya watu na makazi
mwishoni mwa mwaka huu.
Mwenyekiti
wa tume hiyo, Hajjat Amina Mrisho alitoa kauli hiyo alipokuwa akizungumza na
wamiliki wa vyombo vya habari ambako aliwahakikishia kufanyika kwa umakini
mkubwa pamoja na kwamba watachukua muda mfupi wa miezi minne.
Hajjat
Amina aliwaondoa hofu wamiliki hao kwa kuwaambia kwamba wasiwe na shaka na muda
utakaotumika hadi kutangaza matokeo ya Sensa hiyo kama ilivyokuwa ikifanyika
huko nyuma.
Alisema
kutokana na Tume hiyo kujipanga vilivyo ndio maana kuna uhakika wa kupatikana
matokeo hayo haraka na kwa mafanikio pindi zoezi hilo litakapofanyika Agosti 26
mwaka huu.
“Watu
waliolengwa kuhesabiwa katika zoezi hilo ni wale waliolala katika kaya usiku wa
kuamkia Siku ya Sensa, na lengo likiwa kupata idadi ya watu wote waliopo nchini
ikiwa ni pamoja na kukusanya taarifa za kijamii na kiuchumi,” Alisema.
Aliongeza
kuwa kushiriki sensa ni muhimu kwa kuwa kutaipa nafasi Serikali kufahamu
mahitaji ya Wananchi wa kila rika, mahali walipo na watu wenye mahitaji
maalum.
Akizungumzia
kuhusu utoaji wa elimu kuhusu zoezi hilo, Mwenyekiti huyo aliviasa vyombo vya
habari kuweka uzalendo mbele kuliko kulenga maslahi ya kupata matangazo kwanza
kutoka kwenye Ofisi ya Taifa ya Takwimu ya Takwimu.
Hata
hivyo, Kauli hiyo ilionekana kuzua mjadala kwa baadhi ya wamiliki na wandishi wa
habari wa vyombo mbalimbali walioishauri tume hiyo kutobagua baadhi ya vyombo
vya habari kwa kuvipa matangazo.
Walisema
kwamba uzoefu unaonesha kwamba kumekuwa na tabia kwa Idara za serikali kutoa
matangazo kwa kuvibagua baadhi ya vyombo hivyo kitendo ambacho kinawakatisha
tamaa.
No comments:
Post a Comment