Thursday, July 30, 2015

Olesendeka huwezi kuhamia dini nyingine leo na kupewa ukadinali Chadema wangekuwa wavumilivu kwa Lowassa

indexMahmoud Ahmad Arusha
………………………………………
Uvumi ulioenezwa na mitandao ya kijamii kuwa mh.Christopher Ole Sendeka anahamia chadema ameikanusha na kusema kuwa haina tija na niupotoshaji wa jamii na kuwa yeye atabakia kuwa muuumini wa chama cha Mapinduzi wala hajaona chama mbadala zaidi ya chama hicho.
Sendeka ameyasema hayo leo wakati akiongea na vyombo vya habari jijini hapa na kuwataka wanaoeneza kuacha mara moja kumuhusisha na kuhamia kwenye chama hicho kwani yeye ni muumini wa CCM.
Alisema kuwa hajaona chama mbadala zaidi ya chama cha Mapinduzi hivyo yeye ni muumini mzuri wa chama hicho na asihusishwe na kuhamia cha chochote zaidi ya kuwa mwanachama mwaminifu wa CCM.
“Chama sio gulio la kukusanya watu wanaotaka madaraka kwa nguvu bali ni sehemu ya kujadili na kuondoa matabaka kati ya watawala na watawaliwa na kimbilio la wanyonge bila kujali uwezo wake kifedha”alisema Sendeka
Alisema chadema ingebaki salama kama chama hicho kingembakisha mh.Edward Lowasa kuwa mwanachama wa kawaida kwa muda na si mgombea moja kwa moja.
“Huwezi kuingia kwenye dini siku hiyo hiyo nab ado hujashika mafundisho ya dini vizuri ukapewa ukadinali na usheikh hapo hapo hilo litakuwa tatizo kubwa kwa utakaowaongoza hivyo CHADEMA ingevuta subira na kuwapa nafasi wanachama wazoefu wa chama hicho hiyo ndio demokrasia.
Akabainisha kuwa hata ukiwa na hasira leo huwezi kupambana ngumi na Tyson utajikuta umepigwa vibaya katika ulingo kwa kuwa na hasira unatakiwa utafakari na kuondoa jazba iliuweze kudhidhibiti hasira kabla hujaamua.
Sendeka alisema kuwa yeye atabaki kuwa mwanachama wa ccm na kuwa teyari ni mmoja wa wagombea wanaotaka nafasi ya ubunge kwenye jimbo la Simanjiro na kuwa anauhakika wa kushinda kwenye kura za maoni ya chama hicho.
Alisema kuwa kampeni za kumpata mgombea zinaenda vizuri ndani ya chama cha Mapinduzi bila ya kuwa na kukashifiana wala matusi hivyo anawataka wagombea kwenda na mwendo huo yatakaosaidi kuondoa makundi ndani ya chama hicho.

Lowassa achukua fomu Chadema kuchuana na Magufuli, kazi ipo

unnamed (5)
WAZIRI Mkuu wa zamani Edward Lowassa, amechukua fomu kupeperusha bendera ya  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimpitishe kugombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ifikapo Oktoba 25 mwaka huu.
Katika Makao Makuu ya chama chake hicho kipya leo Edward  Lowassa alipokewa na maelfu ya watu waliovalia sare za chama huku wakiimba wana imani naye.
Edward Lowassa aliwasili makao makuu mchana moja kwa moja akaenda ofisi za Katibu Mkuu Dk. Wilbroad Slaa.
Huku akisindikizwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe, Mwanasheria wa chama Tundu Lissu na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu, Edward Lowassa aliingia katika  ofisi hizo katika jukwaa maalumu la kupokea fomu.
Lissu ndiye alikuwa mzungumzaji wa kwanza kwa kuwahakikishia wanachama hawakubahatisha kumpokea Lowassa kwa sababu walifanya utafiti wa kina.
“Kamati Kuu imejiridhisha kwa kushirikiana na viongozi wote wa juu akiwemo Katibu Mkuu na manaibu wake wote wawili, Mwenyekiti na makamu wote wawili, wajumbe wa Kamati Kuu na Mkutano Mkuu, kuwa Edward Lowassa ndiye kiongozi tunayemtaka hivyo Jumapili iliyopita tuliitisha Kamati Kuu ya dharura kumpitisha,” alisema Lissu.
Baada ya kukabidhiwa fomu aliyolipiwa na wanachama waliochangishana fedha  hadi kufikia Sh milioni moja, Edward Lowassa alisimama kuwasalimia waliohudhuria kwa kuwaahidi kufanya kazi kwa juhudi ili kuiondoa Tanzania katika hali mbaya ya kiuchumi.
“Nashukuru kwa kunipa heshima kubwa namna hii, sina maneno ya kuwashukuru zaidi ya kuahidi kufanya kazi kwa bidii ili iwe malipo ya mlichonifanyia.
“Shukurani yangu itakuja baada ya kushinda uchaguzi, lakini ushindi hauji bila umoja. Chadema inaweza kuleta mabadiliko kupitia ukawa.
Baada ya kumaliza kuzungumza alisimama Mbowe kutoa neno la shukurani kwa Edward Lowassa kwa kusema Chadema kitaendelea kuwa chama makini kinachosimamia maamuzi yake.
Vilevile alizungumzia ratiba ya vikao vya kujadili fomu ya mgombea ambaye mpaka sasa ni Edward Lowassa pekee, “Vikao vitaanza Agosti mbili kujadili namna tutakavyoingia katika uchaguzi mkuu.
“Baraza Kuu litaketi Agosti tatu kujadili fomu ya mgombea na kujadili ilani ya uchaguzi, Mkutano Mkuu utafanyika Agosti nne kupitisha jina la mgombea na mgombea mwenza.
“Vikao vya kamati  Kuu vitaendelea tarehe tano, sita hadi saba kuidhinisha wagombea wa ubunge kwa kushirikiana na Ukawa. Kazi ya kujadili wagombea si ndogo nawaomba waandishi wa habari muwe wavumilivu msipige ramli,” alisema Mbowe.
Baada ya kumalizika hafla hiyo Edward Lowassa alitoka nje kwa ajili ya picha ya pamoja kuwaonyesha wanachama fomu yake.

Tuesday, July 28, 2015

Yaliojiri ziara ya Obama Kenya

17.10pm:-Nchini Burundi nawataka viongozi kuketi chini na kujadiliana ili kupunguza umwagikaji wa damu wa aina yoyote.Kenya vilevile itashirikiana na Marekani katika kukabiliana na magonjwa ili kuzuia milipuko.Serikali haifai kuwatenga watu kulingana na jinsia zao kwa kuwa wao wana haki kama watu wengine.
Obama
17.01pm:-Tishio la Ugaidi-wakenya wameonyesha uvumilivu wa kukabiliana na tatizo hilo.Tunaishukuru Kenya kwa kuwahifadhi wakimbizi wengi wa Somalia.Tumezungumza kuhusu kukabiliana na itikadi kali.Mataifa yetu yatafanya kazi kwa ushirikiano mkubwa ili kufanikiwa
16.55pm:-Pia tunampango wa kushirikiana na serikali kuleta umeme katika maeneo ya mashamabani.kwa pamoja tunakabiliwa na tishio la maendeleo, nampongeza rais Uhuru kenyatta kukabiliana na Ufisadi.
16.53pm:-Ndege za moja kwa moja kutoka Marekani hadi Kenya-Tunataraji kwamba hili litaangaziwa na safari hizo kuanza hivi karibuni,lakini kuna baadhi ya maswala ambayo ni sharti yaangaziwe ikiwemo mambo ya usalama kabla hilo kutimizwa.Tutaongeza makubaliano yetu ya Agoa kwa miaka mingine kumi ili kuimarisha uhusiano wetu wa kibiashara.
16.50pm:Barrack Obama
Obama
Mazungumnzo yetu yanahusisha maslahi ya mataifa yetu.Mwanzo naipongeza Kenya kwa kuimarisha demokrasia nchini.Uchaguzi uliofanyika ulikuwa wa ushindani mkubwa na wa amani.Nitakutana na wawakilishi wa vyama vya kijamii kwa kuwa wao ni kitengo muhimu katika kupigania demokrasia.Vita dhidi ya wawindaji haramu-tuna mpango wa kuweka sheria inayopiga marufuku uuzaji wa pembe za ndovu.Hali ni mbaya nchini Sudan,tunataka vionbozi wa taifa hilo kuweka taifa mbele.
16.47pm:-Marekani na Kenya zina utamaduni tofauti na kwamba kuna maswala muhimu yanayowaathiri wakenya kama vile afya ya uma njaa na umasikini,maswala ambayo yanapewa kipao mbele.Swala la wapenzi wa jinsia moja sio swala muhimu na haliwezi kupewa kipao mbele.
16.46pm:Uhuru-Hatuungi mkono wapenzi wa Jinsia moja
Uhuru Kenyatta
Tunazungumza kwa sauti moja kuhusu maswala mengi sana.Walio katika nyadhfa serikalini ni lazima wawajibike.Tumekubaliana kushirikiana katika mambo mengi ikiwemo kilimo,miundombinu na kawi kwa lengo la Kuimarisha mazingira yatakayovutia uwekezaji.
16.45pm:Obama na Uhuru wajitokeza kuhutubia vyombo vya habari
16.10pm:Mkutano na wanahabari
Ikulu
Mkutano na vyombo vya habari kufanyika mda wowote kuanzia sasa
15.25pm:-William Ruto anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita katika mahakama ya ICC mjini the Hague.
15.30pm:Ruto na Obama
Ruto
Hatimaye naibu wa rais wa Kenya William Ruto amefanikiwa kusalimiana na rais wa Marekani Barrack Obama baada ya kukosekana hapo jana katika ujumbe uliomkaribisha rais huyo alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.
15.15pm:Mkutano na wanahabari
Umati uliomsubiri Obama barabarani
Baada ya kikao hicho cha faragha kati ya serikali ya Kenya na Marekani Viongozi wa mataifa hayo Rais Barrack Obama na Mwenzake wa Kenya watafanya mkutano na wanahabari ili kuweza kutangaza yale walioafikiana katika mkutano huo wa kibiashara
15.00pm:Ikulu ya rais Nairobi kenya
Ikulu
Mkutano wa faragha wa kibiashara kati ya mataifa ya kenya na Marekani umeanza katika ikulu ya rais nchini Kenya.Rais Barrack Obama na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta wanawaongoza wajumbe kutoka mataifa hayo mawili katika mkutano huo.Swala la ugaidi ni miongoni mwa maswala tata yanayotarajiwa kujadiliwa katika kikao hicho.
Watu waliovalia nguo zenye rangi za bendera ya Marekani
Rais ‪Obama‬ pia anatarajiwa kutia sahihi ya mikataba ya kibiashara na mwenyeji wake rais Kenyatta katika ikulu ya Nairobi
14.30pm:Ikulu ya rais Nairobi
Ruto
Rais Barrack Obama kukutana na naibu wa rais wa kenya William Ruto ambaye anakabiliwa na mashataka ya uhalifu wa kivita katika mahakama ya kimataifa ya ICC katika mazungumzo ya kibiashara kati ya Kenya na Marekani yatakayoandaliwa katika ikulu ya rais
13.50pm:Rais Obama akiweka maua
Obama
Rais Barrack Obama akiweka shada la maua katika eneo la kumbukumbu ya mauaji ya kigaidi katika uliokuwa ubalozi wa Marekani katikati ya jiji la Nairobi
13.25:Memorial Park
Obama
Obama
Rais Obama na Uhuru Kenyatta wawasili katika eneo la shambulizi la kigaidi katika uliokuwa ubalozi wa Marekani katikati ya jiji la Nairobi.Baadhi ya barabara katika jiji la Nairobi zimebakia kuwa mahame
13.10pm:Manusura 1998
Manusura
manusura
Raia Walionusurika shambulizi la 1998 kenya wabeba mabango wakidai kwamba hawakufidiwa.Wanamtaka rais Obama kutowatupa na badala yake kuangalia maslahi yao.
12.45pm:Densi
Wachezaji densi
Nairobi
Wachezaji densi ya kimasai wakisubiri kumtumbuiza rais Barrack Obama aliyetarajiwa kuwatembelea katikati ya jiji la Nairobi
12.30pm:M-kopa
M-kopa
Rais Obama kwa sasa ametembelea maonyesho ya uvumbuzi jijini Nairobi ambapo alikutana na June Muli afisa anayesimamia maslahi ya wateja M-Kopa ambao hutoa huduma ya kawi ya jua ya 'pay as you go' katika makaazi.
11.10am:Memorial Park
Obama-uhuru
Obama na Uhuru sasa waelekea katika eneo la shambulizi la kigaidi la mwaka 1998 jijini Nairobi
10.55am:
Obama na Uhuru
Obama amaliza hotuba yake
10.50am:BBC hewani moja kwa moja
Obama
Runinga ya BBC inapeperusha moja kwa moja kongamano hilo hewani
10.48am:Mpesa
Obama
Kenya inaongoza katika teknolojia za kibiashara.Kwa mfano utumizi wa Mpesa-ni vyema kwamba teknolojia hiyo ilianza hapa Kenya
Obama akiwasikiza wajasiria mali
Obama 'Tutazindua mfuko wa kudhamini biashara zinazoanzishwa na wanawake
Kina mama ndio injini ya maendeleo barani Afrika.
Vibonzo nchini Kenya
Vituo vitatu vitafunguliwa Mali,Kenya na Zambia barani Afrika ili kuwasaidia wanawake wajasiriamali
10.41am:Rais Obama
Rais Obama
Rais Obama awasalimia wakenya kwa neno 'niaje' na
Hawayuni na kusema kuwa familia yake inatoka nchini kenya.
Lengo la mkutano huu aliouzindua miaka mitano iliopita mjini Washington ni kuwapiga jeki wafanyibiashara duniani.
Amesema kuwa kuna umuhimu wa kukabiliana na ufisadi ili biashara kushamiri.
10.35am:Uhuru Kenyatta
Obama
Kenya ilikumbwa na chanagamoto chungu nzima ikiwemo majanga lakini imesimama imara na kusonga mbele.
Bara la Afrika haliwezi kutegemea mataifa ya magharibi .
Taifa la kenya ni chimbuko la makabila tofauti.
Rais Obama
10.15am:Mkutano waanza
Mkutano wa wajasiriamali umeanza katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini Nairobi huku Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta akihutubia mkutano
10.00am:Msafara wa Rais Uhuru Kenyatta
Uhuru Kenyatta
Msafara wa Rais Uhuru Kenyatta ukiwa tayari umewasili katika eneo la mkutano wa wajisiriamali unaotarajiwa kufunguliwa na raia wa marekani Barrack Obama
09.45am:Waandishi
Waandishi habari
Waandishi
Waandishi wa habari wakijiandaa kuliangazia kongamano la kibiashara la wajasiriamali katika eneo la Gigiri jini Nairobi.Vifaa vya waandishi hao vimepekuliwa na maafisa wa usalama wa Marekani.
09.00am:Ndege Nairobi
Ndege za kijeshi
Ndege za kijeshi za Marekani zimeanza kuzunguka katika anga ya jiji la Nairobi kuimarisha usalama.
08.30am:Barabara za Jijini Nairobi:
barabara
Barabara nyingi za mji wa Nairobi zimeonekana kuwa bila watu na magari kufuatia kuwasili kwa rais Obama.Mapema leo maafisa wa polisi walionekana katika barabara zinazoelekea katika eneo la Gigiri ambapo rais Obama atafungua rasmi kongamano la kibiashara.
08.20am:Obama na familia yake
Sara Obama,Barrack Obama na Daktari Auma
Mama Sarah Obama,Rais Obama na dadaake Daktari Auma Obama wakijumuika katika chakula cha jioni katika hoteli moja jijini Nairobi.
CREDIT: BBC