Saturday, February 16, 2013

Kipindi cha Marehemu Reeva kuoneshwa kwenye luninga

Kampuni moja ya televisheni ya Afrika Kusini inasema itasonga mbele na mpango wake wa kutangaza kipindi kinachomuonesha Reeva Steenkamp, mchumba wa mawanariadha mlemavu, Oscar Pistorious.
Teeva Steenkamp, aliyekuwa mchumba wa Pistorius
Msichana huyo alipigwa risasi na kuuwawa nyumbani mwa Bwana Pistorious siku ya Alkhamisi na mwanariadha huyo sasa ameshtakiwa kwa mauaji yake.
Alipouwawa Reeva Steenkamp alikuwa anakaribia umaarufu mkubwa.
Mrembo huyo aliyekuwa na umri wa miaka 29 alikuwa ashiriki kwenye kipindi cha Tropical Island of Treasure ambacho kingetayarishwa nchini Jamaica.
Katika hatua ambayo itaonekana na utata shirika la habari la SABC limeamua kuonesha kipindi kimoja tayari kimesharikodiwa, licha ya mauaji ya Reeva Steenkamp.
Mtayarishi wa kipindi alisema kipindi cha juma hili kitakuwa kumbu-kumbu ya Reeva Steenkamp.
Wakati huohuo mabango yaliyokuwa mabara-barani yanayomuonesha mchumbawake, Oscar Pistorius, yanabanduliwa.
Pistorius bado anazuwiliwa na polisi baada ya kuifikishwa mahakamani Ijumaa.
Ombi lake la kutaka kuachiliwa kwa dhamana litasikizwa Jumanne.

Monday, February 11, 2013

Hivi mapigano haya ya Wakritu na waislamu kuhusiana na machijio ni mpaka lini?


Majeruhi Abdalah Ibarihim akiwa amejeruhiwa vibaya baada ya kukatwa mapnga kichwani na watu wanaodaiwa kuwa ni Wakristo

Huyu naye ni majeruhi aliyetambuliwa kwa jina la Steven Andrea (34) ambaye anadaia kujeruhiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni waislamu,

Mchungaji aliyethibitishwa hadi sasa ni wa kanisa la PAGT aliyetambuliwa kwa jina la Mathayo Kachira(33),Mwili wake umehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti katika hospitali ya wilaya ya Geita.

Thursday, February 7, 2013

Watakiwa kuwajali wanamgambo wanaozuia magendo ya kahawa maeneo ya mipakani-Massawe



Na Theonestina Juma, Kagera
MKUU wa mkoa wa Kagera Kanali Fabian Massawe ameutaka uongozi wa Wilaya zote za mkoa Kagera kuhakikisha wanawawezesha wanamgambo wanaokuwa kwenye vizuizi vya mipakani ili kuthibiti magendo ya kahawa  yanayo likosesha Taifa mapato.
Kwa mujibu wa   Kanali Massawe Mgambo hao wanawekwa kwenye vizuizi kwa lengo kuzuia magendo ya kahawa  ambapo miaka ya nyuma waliweza kuokoa zaidi ya bilioni 1.9 wakati huo hawakuwezeshwa  kwa chochote unategemea.
“Hawa wanamgambo kipindi cha nyuma waliweza kuokoa kahawa yenye thamani y ash. bilioni 1.9  bila kuwezeshwa na kwa chochote kile hivi mnadhamani kuwa wataendelea kuzuia wakati wana njaa? Alihoji na kusema matokeo yake wataanza kupokea rushwa na kuruhusu kahawa ivushwe na kupelekwa nje ya nchi na kulikosesha Taifa mapato”alisema Massawe
 “Naagiza kama mnataka magendo ya kahawa iishe na tuweze kuongeza pato la Taifa tuhakikishe tunawalipa walinzi hao,tuwawezeshe kujiepusha na vitendo vya rushwa kwani  kati ya bil. 1.9 walizookoa mkitoa milioni 40 mkawalipa mnapungukiwa nini ?alihoji  na kuongeza
“Ukitaka kupata pesa lazima utumie pesa ,ila mkiambiwa hivyo mnadai kuwa Wilaya na Halmashauri hazina pesa mbona mkiitwa kwenye vikao na Semina Dar es Salaam pesa ya kupanda ndege haikosi?kwa hiyo na hiyo itafutwe hatuwezi kukosa mapato hivi hivi mwaka jana kahawa nyingi imevushwa nje mwaka huu hatutaki kusikia ikivushwa “alisema.
 Katika hatua nyingine mkuu huyo aliwataka watendaji wote wa Serikali mkoania hapa kutochanganya kazi na Siasa badala yake wafanye kazi kwa kufuata viapo vyao walivyotoa wakati wakiomba kazi ili kuwaletea maendeleo wananchi.
 Alisema kuwa Mkaguzi mkuuwa Serikalia anakuja mkoani humo anataka kukuta mambo yote yakiwa sawa kwa hiyo “Nawatahadharisha watendaji wanaorudisha nyuma maendelo kwa maksudi kwa kushindwa kumaliza miradi ya maendeleo wakati pesa nyingi yha Sarikali imetolewa kwa kisingizio ati sikitaki chama cha mapinduzi wasichang’anye kazi na siasa wachague moja.
 “Kuna watendaji wanatuhujumu kwa kurudisha nyuma maendeleo kwa sababu ya itikadi zao za vyama vya siasa hiyo ni dhambi hatuwatendei wananchi haki zao kwani wao ndio waajiri wetu tunapokea mishahara kutokana na kodi zao tuweke pembeni siasa tufanyekazi tuache malumbano penye vurugu za kidini au siasa hapawezi kuwa na amani wala maendeleo”alisema
 Asema kuwa tofauti za kisiasa kati ya watendaji na madiwani imekuwa ikisababisha miradi mingi kutokamilika kwa wakati na mingine kukwama kabisa kwa hiyo sheria ndogo zitumike kuwabana hao wasiojua kuwa maendeleo ni nguzo muhimu katika Taifa letu.
Mwisho