Monday, December 8, 2014

Amezwa na nyoka ili kukamilisha uchunguzi wake tumboni mwaAnaconda


Nyoka wa Anaconda hupatikana zaidi katika msitu wa Amazon
Watu nchini Marekani wameelezea ghadhabu na hasira zao kwenye mitandao ya kijamii kufuatia utafiti wa mtaalamu wa wanyamapori Paul Roslie kumezwa na Nyoka aina ya Anaconda ili ku chunguza maumbile ya ndani ya Nyoka huyo.
Lengo la utafiti huo ambao ulikuwa wa kwanza wa aina yake duniani, ilikuwa ni kuchunguza maumbulie ya ndani ya Nyoka huyo anayepatikana katika msitu wa Amazon.
Hata hivyo inaarifiwa bwana Paul alilazimika kusitisha utafiti wake ambao umezua utata muda mfupi tu baada ya kuuanzisha.
Watu nchini Marekani walijionea kwenye televisheni zao kipindi kilichokuwa kinapeperushwa cha mtaalamu huyo kuingia ndani ya tumbo la Anaconda akiwa amevalia vazi maalum ambalo yangesaidia kuchunguza kiwango cha joto mwilini mwake na pia kupima mipigo ya Moyo wake wakati akiwa ndani ya tumbo la Nyoka huyo.
Paul na vazi alilotumia kuingia ndani ya Nyoka kabla ya kushindwa na kusalimu amri
Rosolie na kikundi cha wasaidizi wake walipata Nyoka ya Anaconda mwenye uzito wa kilo 180, walipokuwa katika msitu huo. Alipanga kuwa ataonyeshwa kwenye stesheni hio akiwa anamezwa mzima mzima na Nyoka huyo.
Rosolie alionekana akiingia ndani ya mdomo wa Anaconda kwa kichwa chake huku wenzake wakimtazama.
Alikuwa amevalia vazi maalum lenye Carbon na likiwa limepakwa damu ya Nguruwe, kabla ya kujielkeza kwa Nyoka huyo kama mlo wake.
"sikutana kumhangaisha mno mnyama na pia mimi mwenyewe sikutaka kujiumiza. ''
Paul anapenda sana kujihusisha na maswala ya wanyama hasa Nyoka
"nilitaka kuhakikisha kuwa vazi langu halitamjeruhi Nyoka huyo kwa vyovyote vile.''
''Mimi mwenyewe sikuogopa hata kidogo. Watalaamu walifanyia jaribio vazi langu, kwa hivyo tulijua kuwa halitamwathiri kwa vyovyote Nyoka huyo. ''
Lakini baada tu ya saa moja ya mtaalamu kuingia ndani ya tumbo la Nyoka na kuanza kubanwa, aliamua kusitisha utafiti wake akihofia kuwa angeumizwa na Nyoka huyo mkubwa. Alisikika akiwaita wenzake kwa kifaa maalum cha kupaza sauti kilichokuwa kimewekwa kwenye vazi lake na kuwamabia kuwa anaumizwa.
''Nahisi kama mifupa yangu inasagwa sagwa, njooni mniondoe hapa.'' alisema Paul.
Namna ambavyo Rosolie aliponea kufa baada ya kubanwa na Nyoka huyo bado ni muujiza ingawa aliweza kupata hewa kutokaa kwa vazi lake hilo kwa saa tatu.

Idris wa Tanzania aibuka kidedea Big Brother 2014

Idris Sultan mshiriki wa mashindano ya Big Brother ‘hotshots’.Toka Tanzania ameibuka kidedea wa mashindano hayo yaliyokua yakifanyika nchi Afrika Kusini.
Idris amekua Mtanzania wa pili kushinda shindano hilo ,baada ya Richard Dyle Bezuidenhout; kuibuka shujaa mwaka 2011 katika Big Brother II.
Mshindi huyu anajinyakulia donge nono la Dola za marekani laki tatu,kwa kuibuka mshindi.
Tayo Faniran toka Nigeria amekuwa mshindi wa pili katika mashindano hayo .
Idris alitabiriwa na wapenzi wa kipindi cha Bigbrother kuwa angeweza kuibuka mshindi kutokana na wadau wengi kuvutiwa na namna alivyokuwa akiishi katika jumba hilo la big brother pia uhusiano wake na washiriki wenzake.

Wednesday, November 26, 2014

Ripoti ya ESCROW yatikisa nchi, inasikitisha!!

Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Zitto Kabwe akiongozana na Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini,Mhe. Ismail Aden Rage wakati akiwasili bungeni kuwasilisha Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (GAG) kuhusu akauti ya ESCROW.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anne Makinda akifafanua jambo wakati akiendesha Bunge hilo leo mjini Dodoma.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe Zitto Kabwe akienda kusoma Ripoti ya GAG kuhusu akauti ya ESCROW.
Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali Mhe Zitto Kabwe akisoma Ripoti ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (GAG) kuhusu akauti ya ESCROW Bungeni Mjini Dodoma leo.
Waheshimiwa Wabunge wakimsikiliza Mhe. Zitto Kabwe (hayupo pichani) wakati akisoma ripoti ya CAG.
Baadhi ya wahudumu wa Bunge wakigawa Ripoti ya GAG kuhusu akauti ya ESCROW kwa Wabunge
Waheshimiwa Wabunge wakipitia ripoti ya GAG kwa makini wakati ikisomwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali, Mhe Zitto Kabwe.
Baadhi ya waandishi wanaoripoti habari za Bunge wakifuatilia mjadala kwa makini.
Naibu katibu wa Bunge, John Joel akijadiliana jambo na Mhe. Spika Anna Makinda.
Wabunge wakiwa wamesimama kuashiria kuunga mkono taarifa iliyosomwa Bungeni leo na Mhe. Zitto Kabwe.
Mhe Said Arfi akimpongeza Mhe.Zitto Kabwe ,mara Baada ya kumaliza kusoma ripoti ya GAG.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali,Mhe DEO Filikunjombe akiwasilisha maazimio ya kamati yake.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Mhe. Anne Makinda akitoka ndani ya Ukumbi wa Bunge mara baada ya kuahirisha Bunge mpaka kesho ambapo Serikali inatarajiwa kutoa majibu.
Naibu Waziri wa Nishati na Madini,Mhe. Stephen Masele akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya Bunge kuahirishwa. Picha zote na Deusdedit Moshi wa Globu ya Jamii kanda ya kat

Friday, November 21, 2014

Mapinduzi KCU 1990, Wajumbe wa bodi wa zamani wote watupwa wachaguliwa sura mpya






Pichani ni wajumbe saba waliochaguliwa leo katika Uchaguzi Mkuu maalum uliofanyika mjini  Bukoba, ambapo mwenyekiti mpya ni Bw. Frank Muganyizi mwenye masters ya Uchumi.

Wednesday, November 19, 2014

Majonzi Bukoba, Mfanyabiashara Maarufu afia ndani ya gari akifanya mapenzina msichana



Na Theonestina Juma,Bukoba
 MFANYABIASHARA  maarufu  mjini  Bukoba Mkoani Kagera, Bw.Leonard Mtensa (50) amefariki  dunia ghafla  wakati  akifanya mapenzi na mwanamke mmoja  ndani ya  gari  lake.
Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mjini hapa na kusambaa kila kona ya mji wa  Bukoba nakuthibitishwa na  Kamanda wa polisi Mkoa Kagera Henry Mwaibambe ,tukio hilo la aina yake limetokea Novemba 18,mwaka huu saa 4.00 usiku katika maeneo ya Buyekera mjini Bukoba
Kamanda  Mwaibambe,alisema mfanyabiashara huyo ni  mmiliki wa klabu  maarufu  ya   usiku  Bukoba   iitwayo  Linas night club.
Alisema kabla ya   kufikwa  na  umauti  mfanyabiashara huyo  alikuwa akifanya mapenzi ndani ya gari  lake  lenye namba za usajili T.982 CQG  aina  ya IST.
Alimtaja msichana aliyekuwa akifanya mapenzi na mfanyabiashara huyo kuwa ni Bi. Jackline  Hassan (25 )  mkazi wa Buyekera.
Alisema  wakati  wapenzi  hao  wakiendelea  na mapenzi  ghafla   hali   ya mfanyabiashara  huyo   ilibadilika  na kukimbizwa   katika  kituo  cha   Afya cha  ELCT  Ndolage  kilichopo   Bukoba lakini  alifia njiani.
Alisema baada ya gari lake kupekuliwa  kulikutwa na vilevi mbalimbali  ikiwemo Whisky aina ya Bond 7 aliyokuwa anakunywa.
Alisema jeshi la polisi mkoani hapa linamshikilia, Bi. Jackline kwa ajili ya kusaidia upelelezi na kuwa chanzo cha kifo hicho hakijajulikana