Friday, June 20, 2014

Mahakama ya mkoa Kagera yawafuta kazi madiwani saba wa Manispaa ya Bukoba

Na Theonestina Juma, Bukoba
 MADIWANI sita  kati ya tisa waliokuwa wanashtakiwa kwa kosa la kushindwa kududhuria vikao vya vya Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera wamevuliwa vyadhifa zao na Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Kagera.

Akisoma hukumu hiyo leo mbele ya Mahakama hiyo,Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Charles Uiso, alisema madiwani hao wanavuliwa udiwani huo kutokana na mahakama hiyo kuidhika na ushahidi wa pande ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.

Ilielezwa mahakamani hapo kuwa madiwani hao,walikuwa wakikataa kuhudhuria vikao vya baraza la madiwani pamoja na vikao mbali mbali vya baraza hilo jambo lilisababisha kurudisha nyuma  maendeleo ya wananchi wa manispaa ya Bukoba.

 Uiso amesema kuwa ushahidi wote uliotolewa mahakamani hapo umeweza kuridhisha mahakama bila kuwa na shaka lolote.

Madiwani waliovuliwa nafasi zao za udiwani ni pamoja na Bw. Samuel Ruangisa kata Kitendaguro(CCM) Bw.,Deusdedith Mutakyahwa kata Nyanga(CCM,),Bw.Yusuph Ngaiza kata Kashai(CCM),Bw.Dauda Kalumuna kata Ijuganyondo (CC) , Bi. Murungi Kichwabuta Viti maalumu(CCM)na Rabia Badru viti maalumu (CUF).

Hata hivyo, mahakama hiyo imetupilia mbali malalamiko dhidi ya madiwani wengine wawili Bw. Richard Mwemezi kata Miembeni(CCM)na Bw.Israel Mlaki kata Kibeta(CHADEMA) kwa madai kuwa  hawa hawahusiki moja ka moja na malamiko hayo kwani na kwa Bw.Richard kuwa  hakuwa mjumbe wa kamati hiyo na Israel Mraki aliweza kuhudhuria baadhi ya vikao hivyo.

 Kutokana na hali hiyo  Mahakama imewaamuru madiwani hao saba  waliovuliwa  udiwani kulipa gharama za uendeshaji wa kesi hiyo kwa mlalamikaji.

Hukumu ya kesi hiyo iliyotumia takribani masaa mawili, ilivuta hisia za watu na kuwafanya wagawanyike katika pande mbili zilizowahusu wafuasi wa mbunge wa jimbo la Bukoba mjini Hamis Kagasheki(CCM) na aliyekuwa Meya wa Manispaa hiyoDkt.  Anatory Amani,ambavyo mvutano wa makundi hayo yalianza kuibuka mara tu baada ya kuwepo malumbano dhidi ya vigogo hao wa kisiasa.

kesi hiyo ilifunguliwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Afya, elimu na uchumi Bw.Chief Kalumuna, ambaye pia ni diwani wa kata Kahororo(CCM)  ambapo madiwani hao ambao walikuwa wajumbe wa kamati yake walikaidi  kuhudhuria vikao zaidi ya tano.

Alitaja baadhi ya vikao walivyotakiwa kukaa na tarehe kuwa ni pamoja na   Julai 19, Agosti 1,septemba 23,novemba 11 na novemba 14 mwaka 2013.

MWISHO