Na Theonestina Juma
IMEELEZWA kuwa njia moja kubwa ya
kushiriki katika kulitunza Ziwa Victoria ni upashanaji wa habari.
Kauli hiyo imetolewa leo na Afisa
Utumishi wa Mkoa Kagera, Bw.Richard Kwitega kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa Kagera
Kanali Fabian Massawe wakati akifungua semina elekezi ya uhifadhi wa mazingira ya Ziwa Victoria awamu ya pili ya
bonde la Ziwa hilo inayohudhuriwa na viongozi wa Halmashauri naManispaa
zilizo ndani ya bonde la ziwa hilo inayofanyika katika ukumbi wa Kolping mjini
hapa.
Alisema njia hiyo ikitumika
itarahisisha hatua za haraka zikuchuliwe kila inapobidi, kuokoa bayoanuai ya
ziwa hilo ambalo ndilo tegemeo kubwa la wananchi wa maeneo hayo.
Alisema viongozi wanatakiwa kusimamia
na kuhimiza juhudi za kuhifadhi rasilimali za ziwa Victoria kwa kuzingatia
mbinu zote za kutunza na kuhifadhi mazingira na rasilimali zake ili uhai
uwe wa uhakika na wa kudumu.
Bw.Kwitega alisema Ziwa Victoria ni
rasilimali muhimu katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na lina hazina
kubwa zaidi ya samaki wa maji baridi duniani.
Alisema samaki wa thamani kubwa
wanapatikana katika ziwa hilo na wanailetea nchi kipato kupitia soko la ndani
na nje ya nchi hivyo ni jukumu la watu wote kulilinda.
Alisema inakadiriwa kuwa miaka ya
nyuma kabla ya uharibifu wa ziwa hilo kuanza samaki walivunwa kati ya tani
400,000 na 500,000 kwa mwaka ambapo walichangia pato la taifa takribani dola za
Marekani bilioni 3 hadi 4 kwa mwaka.
"Pamoja na hayo kwa sasa
inakadiriwa mavuno ya samaki yameshuka kufikia tani 243,564
kwa takwimu za mwaka 2010.Semina hiyo ya siku mbili inahudhuriwa na Wenyeviti, Mameya, Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa mikoa ya Geita, Kagera,Mara na Mwanza.
kwa takwimu za mwaka 2010.Semina hiyo ya siku mbili inahudhuriwa na Wenyeviti, Mameya, Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa mikoa ya Geita, Kagera,Mara na Mwanza.
No comments:
Post a Comment