Tuesday, December 31, 2013

Mwenyekiti wa kijiji afungwa maisha jela kwa ubakaji, atupa hirizi mbili akielekea gerezani amtuhumu mganga wake kumdanganya

Na Theonestina Juma, Ngara
 MWENYEKITI wa kijiji cha Kumwendo kata Mbuba Wilayani Ngara, Bw.Paul Rutishobwa (45) amehukumiwa kifungo cha maishajela  na Mahakama ya Wilaya ya Ngara baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka minane.
Hukumu hiyo imetolewa juzi na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Ngara,Bi.Mariam Lusewa baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani.
Awali mwendesha mashtaka wa jeshi la polisi wilayani Ngara, Tumaini Membi aliiambia mahakama hiyo kuwa, Mwenyekiti huyo alitenda kosa hilo, Septemba 18, 2012 saa 2 usiku kijijini hapo.
Alisema siku ya tukio, mtuhumiwa huyo alimwita mtoto huyo akiwa nyumbani kwao kwa lengo la kumtuma, ndipo alipomkamata na kumziba mdomo na kumvutia kwenye shamba la mihogo na kuanza kumbaka.
Alisema mtuhumiwa huyo alimvuta mtoto huyo umbali wa mita kama 15 kutoka nyumbani kwao  ulikuwa na shamba la mihogo na kuanza kubaka.
Alisema mama wa mtoto huyo, Bi.Pelagia Gwassa
kwa wakati huo alikuwa akipika jikoni na alipomaliza shughuli za
mapishi ndipo alianza kumtafuta mwanae aje ale bila mafanikio, ndipo alipiga makelele kuwaita majirani ili wamsaidie kumtafuta
mwanae.

Alisema baadhi ya wananchi walijikusanya kuanza kumtafuta, ambapo walipofika kwenye shamba hilo la mihogo walisikia sauti ya mtoto huyo akisika kama anagugumia kwa maumivu.
Alisema walipomkaribia walimkuta akiwa anachuruzika damu kutoka sehemu zake siri huku akiwa amefungwa mdomo kwa kitambaa.
Alisema alipoulizwa amekuaje, alimtaja Bw.Rutishobwa kumvua nguo na kumwingilia na kisha kumwacha hapo.
Mtoto huyo alipelekwa katika hospitali ya Mabawe na kubaini kuwa amebakwa na kufikishwa mahakamani ambapo kipindi hicho chote alikuwa nje kwa mdhamana.
Hata hivyo, kwa upande wa mtuhumiwa akijitetea alidai kuwa hakumbaka mtoto huyo bali anasingiziwa.
Bw.Rutishobwa aliwaacha hoi mahakama hiyo baada ya kuhukumiwa maisha kwa kutoa hirizi mbili katika mkono wake wa kulia na kushoto na kuzitupa chini akidai kuwa mganga alimdanganya kuwa hatafungwa.
Hata hivyo, habari zaidi zinaeleza kuwa Bw. Rutishobwa, aliwahi kuoa dada yake baba yake mtoto aliyebakwa, na kuzaa nae watoto wanne,na baadaye kutengana na hivyo mtoto aliyembaka alimzoea kwa sabbau ya undugu huo.

Kanisa Katoliki Ngara latishia kusitisha kuwabatiza watoto wa kiume

Na Theonestina Juma, Ngara
UONGOZI wa Kanisa Katoliki Parokia ya
Ngara Mjini umetishia waumini wake kusitisha kuwabatiza watoto wao wa kiume wasipobadilika katika kuwabagua watoto wao katika kuwajenga kiimani.

 Tishio hilo limetolewa jana na Paroko wa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Fransisco wa Asizi Parokia ya Ngara Mjini, Ivus Tindyebwa wakati akihubiri kanisani hapo ikiwa ni siku ya familia ilioenda sanjari na ubatizo wa watoto zaidi ya 40.
 Kwa jinsi hali ilivyo katika malezi ya  watoto,wazazi wengi wamekuwa wakiwalea watoto wao kimfumo dume, watoto wa kike wakiwa ndiyo wanawajibishwa zaidi huku watoto wa kiume wakiwa hawahimizwi hata kidogo kujishughulisha na masuala ya dini.
 Hatua ya Paroko huyo kusema hayo ni kutokana Jumamosi Desemba 28, mwaka huu jimbo la Rulenge liliadhimisha siku ya utoto Mtakatifu,
wilayani Biharamulo na cha kushangaza watoto wa kike ndiyo walikuwa wengi kana kwamba siku hiyo ilikuwa ni utoto wa usichana."

 "Itafikia hatua sasa siku ya utoto mtakatifu tutabadili iwe siku ya usichana mtakatifu, kwa sababu siku hiyo inayowalenga watoto wa jinsi zote na si watoto wa kike pekee"alisema Paroko huyo.
Aidha  alihoji sababu ya waumini wa kanisa hilo kuegemea kwa watoto wa kike pekee na kuendelea kutoa malezi ya kiroho kiubaguzi uliojaa mfumo dume?
Hata hivyo alisema tatizo la kutoa malezi ya kiroho kiubaguzi haliko wa Jimbo la Runge tu bali ni tatizo kwa nchi nzima na hivyo ni wajibu wa waumini wa kanisa hilo kubadilka katika malezi ya watoto wao kiroho.
 Alisema "wakristo wanatakiwa kubadili mfumo wa ulezi wa watoto wao kiroho kwa kuwahusisha watoto wa jinsi nzote".
 Alisema licha ya wakati wa ubatizo hata majina ya watoto wa kiume yanakuwepo lakini anashangaa ikifika wakati wa huduma kanisani watoto wa kiume hawajitokezi na badala yake watoto wa kike ndiyo wanaonekana wengi.
 Katika hatua nyingine Paroko huyo aliwakata vijana wa kanisa hilo kuachana na ndoa za kuwavuta kwa nguvu wasichana kwani inawafanya kuingia katika sakramenti hiyo bila kuchunguzana, kama wamekomaa kiakili na kimwili katika kulea familia yao kiroho.
Alisema wale wanaoingia katika ndoa kwa mfumo huo mwishoe ndoa yao inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kutengana baada ya kujigundua kuwa hawawezi kuishi pamoja, jambo ambalo ni changamoto kwa kanisa.
 

Monday, December 23, 2013

Wahamiaji haramu waliorejeshwa makwao na Operesheni kimbunga warudi Kagera, watishia wananchi,wawapora mali, wajiita M23



Na Theonestina Juma, Kagera
KATIKA hali isiyo ya kawaida wahamiaji haramu waliorejeshwa nchini mwao na serikali ya Tanzania kwa operesheni  kimbunga wamerejea kwa uwingi wilayani Kyerwa na kuwatishia wananchi kwa kujiita M23 na kuwapora mali zao kwa nguvu.
Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa wilaya ya Kyerwa, Mhandisi Benedict Kitenga  wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera kanali, Massawe aliyembelea wilayani hapo  kukagua maendeleo pamoja na ujenzi wa mabara ya shule za sekondari za kata.
Alisema kutokana kurejea kwa kasi ya ya ajabu kwa wahamiaji haramu katika kijiji na kata ya  Kibingo na kuwatishia wananchi wa kijiji hicho kwa kujiita M23 kunawatia hofu wananchi hao.
“Wahamiaji hao walikuwa wametengeneza makambi na kujihami kwa mapanga na marungu pia walikuwa wakipita katika kijiji hicho na kuwatishia wananchi na kuwanyanganya  chakula kwa nguvu pia kuwatishia maisha yao”alisema.
Hata hivyo, Mkuu huyo wa wilaya alisema baada ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya kupata taarifa hizo walikwenda katika eneo hilo na kufanya operesheni kubwa na kuwakamata wahamiaji haramu zaidi ya 20 pamoja na  baadhi ya Watanzaia ambao walikuwa wakishirikiana na wahamiaji haramu hao kuwahifadhi.
Alisema Wahamiaji haramu hao waliokamtwa walirejeshwa kwenye nchi zao bila kutaja uraia wao na watanzania walihusika walichukuliwa hatua kali za kisheria.
Kutokana na hali hiyo, alisema wananchi wanatakiwa kutoa taarifa mara wawaonapo hao wahamiaji haramu wakirejea au katika maeneo yao
Hata hivyo, kwa upande wa Mkuu wa mkoa Kagera, kanali Fab ian Massawe alisema katika operesheni Kimbunga waliondolewa wahamiaji haramu 31,000 badala ya 52,000 kwa hiyo operesheni hiyo inaendelea ili kuhakikisha waliobaki wanaondolewa na hakuna wa kurudi nchini.
“Chini  ya Kaulimbiu ya Hakuna wa Kubaki na Hakuna wa Kurudi, tutahakikisha kila mhamiaji haramu anaondoka na watanzania watakogundulika kushirikiana nao watachukuliwa hatua kali za kisheria, pia naagiza Kamatia za Ulinzia na Usalaama kundelea na operesheni hiyo mpaka kuwamaliza wahamiaji haramu.” Alisistiza Mkuu wa Mkoa.
Mkuu wa mkoa alisema ili kushughulikia tatizo hilo kikamilifu wananchi wanatakiwa kutoa taarifa hasa kwa viongozi wa juu mfano kwake na mkuu wa wilaya ambapo alitoa namba za simu zake kwa wananchi pamoja na mkuu wa wilaya ili kupambana na tatizo hilo.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi waliohojiwa walisema tatizo la wahamiaji haramu linasababishwa na baadhi ya watendaji wa serikali katika ngazi za chini ambao wanachukua hongo na kuwarudisha katika mazingira ya wananchi.
Wananchi hao walisema inavyoonekana, viongozi wa chini kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji hadi kata wamepewa mamnlaka makubwa mno na pia wamekuwa wakikaa muda mrefu bila kubadilishwa vituo vya kazi na hivyo kujenga mazoea na wahamiaji haramu hao.
“Kinachoitakiwa kifanyike ni serikali kuanzia ngazi ya wilaya kuanza tabia ya kuwatembelea viongozi wa serikali za vitongoji hadi kata kwa kushtukiza ili kuweza kutokomeza hii tabia iliojengeka mikongoni mwao na kuonekana kama miungu watu katika maeneo yetu’alisema mwananchi mmoja.
Operesheni kimbunga iliendeshwa hivi karibuni na serikali kwa kushirikisha vyombo  mbali mbali vya usalama baada ya Rais Kikwete kutoa wiki mbili kwa wahamiaji haramu kuondoka nchini.

Friday, December 20, 2013

Waziri Kaghasheki atangaza kujiuzulu, mawaziri wengine watatu nao wafutwa kazi na Rais Kikwete


kagashekiWaziri wa Maliasili na Utalii Mh. Balozi Khamisi Kagasheki ametangaza nia ya kujiuzulu wadhifa wake dakika chache zilizopita bungeni  mjini Dodoma,sababu kubwa ya kujiuzulu ni baada ya kusomwa  ripoti ya kamati ya Bunge Kumtuhumu kuzembea na kukithiri kwa vitendo viovu vilivyofanywa na wanausalama wakati wa Operesheni Tokomeza.
Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imebainisha kuwa oparesheni Tokomeza Ujangili iliyoendeshwa na Serikali ilikumbwa na unyanyasaji mkubwa wa wananchi, Ukatili, Udharirishaji, Ubakaji na Mauaji huku baadhi ya wazazi wakivuliwa nguo, kuteswa na kubakwa mbele ya wanafamilia.
Akiwasilisha bungeni taarifa ya kamati hiyo Mwenyekiti wake James Lembeli amesema pamoja na mateso hayo yaliyowakumba wananchi pia nyumba zao zilichomwa na mifugo kupigwa risasi huku mingine ikifa kwa kukosa maji, chakula na maziwa kwa ndama wadogo.
Kamati hiyo pia imebainisha kuwepo kwa vitendo vya Rushwa vilivyotawala oparesheni Tokomeza ambapo pia wananchi waliokuwa na mifugo walitozwa faini na mifugo mingine kuuzwa kwa bei nafuu ambayo haikulingana na faini iliyokuwa ikitoza na wafugaji walizuiwa kushiriki mnada wa uuzaji wa mifugo hiyo.
Mbali na Waziri Kaghasheki mawaziri wengine watatu walioonekana kuwa wagumu kutamka na vinywa vyao kuwa wanajiuzulu, wamefukuzwa kazi na Rais Jakaya Kikwete katika taarifa yake iliotolewa mbungeni humo leo na Waziri mkuu Mizengo Pinda baada ya kuwasiliana na naye akiwa nchini Marekani na kumwelezea Rais yote yanayojiri humo mjengoni.

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEizfl9xTIA4YGERZa1hVrvMViAIO-CyQBxGTItNYudwN8nFpnZxwHfJ7n0abKNJWsUmRIFSIxMPdydixs0lVhe-yhifLDDzcRU6GJwfJza8uuKqAy3Vgrc9sbTOydu_S22GAo3uhWOIS3g/s1600/11_10_y7kr7s.jpg












 WWaziri wa Emmanuel Nchimbi aliyewajibishwa na Rais Kikwete
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgNp4eU6V6cPgh_0OiQzpvPpnhm4clZ226qs0Wq5OFxrTezYis2uy0KT04Yn6hWdm6zwRKYildGn18-Du467Pxz47S2nEvOeCtlnf1UhToYEsGadRtnFZuIhAxPTDaGXtjjtRkjWdu1aMM/s1600/26e22-HERM8393.JPG
Waziri wa Uvuvi na mifugo, Dkt. David Mathayo
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhOIzcgR7QpKv0kYsIIJiMImojfMm7-xPx2aL0DnQa1RUGibWv0MBdBjVeR_s46vzj4hggONK8xROOk1sQHTbYH2NJGpaGJdM_yzbxDtTWLpHs-6gtrcmNCZPwB5l1pBZGjW_J84YVSqVg/s1600/nahodhafinger1-e1334564790445.jpg
Waziri wa Shamsa Vuai Nahodha









Tuesday, December 17, 2013

Kijijini Qunu kwao Nelson Mandela kulivyo

Qunu ni kijiji kidogo katika jimbo la Eastern Cape la Afrika Kusini, kilomita 32 Kusini-Magharibi ya mji wa Mthatha, katika barabara ya Butterworth na Mthata. 
Kijiji cha Mvezo, pembezoni mwa mto Mbashe, ni jirani na mahali ambapo Mzee Nelson Mandela alizaliwa. Hapo Qunu ndipo alipokulia na aliweka nadhiri ya kurejea. 
Kijiji cha Qunu ndipo baba yake Mandela alipohamia baada ya kuvuliwa Uchifu wa Mvezo. Katika kitabu chake cha ‘Long Walk to Freedom’ Mzee Mandela amekitaja kijiji hicho kuwa ndipo alipoishi maisha ya furaha wakati wa utotoni. 
Jumapili ya Desemba 15, 2013 Mzee Mandela alizikwa kijijini Qunu katika mazishi ya Kitaifa yaliyoshuhudiwa dunia nzima. Alizikwa kwa heshima zote za kiongozi wa Taifa katika sehemu aliyochagua mwenyewe kuwa nyumba yake ya milele.
 Daraja la waendao kwa miguu likipita juu ya barabara mpya ya lami inayojengwa kuelekea kijijini Qunu.
Siku ya mazishi barabara ya kuelekea Qunu ilifungwa na ni magari yaliyokuwa na kibali tu ndiyo yaliyoruhusiwa kupita
Ulinzi ulikuwa mkali kila sehemu kijijini Qunu
Wageni wakiwa katika geti kuu la nyumba ya Mzee Mandela hapo Qunu
Nyumba ya Mzee Mandela
Nyumbani kwa Madiba kijijini Qunu
Hema maalumu zilikofanyika shuguli zote za mazishi. Kaburi lake liko nje ya hema upande wa kushoto
Hali ilivyokuwa saa kumi na moja alfajiri siku ya Jumapili
Nyumbani kwa Madiba kumejaa magari hata kabla ya jua kupanda angani
Sehemu ya kijiji cha Qunu. Mahema mbele ya nyumba ni ya wanahabari wa kimataifa waliopiga kambi hapo
Mandhari ya Qunu
Mandhari ya Qunu
Ni kijiji chenye mandhari nzuri. Wakati wa majira ya baridi barafu huanguka hapa
Qunu
Kila engo Qunu inapendeza
Kijiji cha Qunu
Bango linalotangaza kijiji cha Qunu kuwa cha urithi
Ulinzi ulikuwa si wa kawaida siku ya mazishi
Foleni ilikuwa ya kufa mtu
Wana Afrika Kusini toka kila kona walitembea umbali mrefu kwa miguu kuhudhuria mazishi
Nyimbo na ngoma vilitawala
Mdau akilipoza koo baada ya kutembea kwa muda mrefu
Sehemu ya mji wa Mthatha, kilomita kama 32 kutoka Qunu
Magari yalizuiwa kwa muda wakati mwili wa Mzee Madiba uliopowasili uwanja wa Mthatha na kupelekwa Qunu
Sehemu ya foleni ya magari ikikaribia mji wa Mthatha na hapa wakisubiri msafara wa mwili wa Mzee Mandela upite

Wednesday, December 11, 2013

Historia ya Rais Mandela yalivyoapanda na kushuka

http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/06/10/130610141417_nelson_mandela_439x549_rexfeatures.jpg 
Nelson Mandela alichaguliwa kuwa rais wa kwanza mwafrika mweusi wa Afrika Kusini,baada ya vita vya muda mrefu dhidi ya utawala wa kizungu.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/06/10/130610144718_nelson_mandela_439x549_rexfeatures.jpg
Alizaliwa mkoani Eastern Cape, lakini baadaye akatorokea mjini Johannesburg ambako alifanikiwa kuwa mwakili na kujiunga na haratakati za chama cha ANC dhidi ya utawala wa kizungu.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/06/10/130610141852_nelson_mandela_439x549_rexfeatures.jpg
Kama kijana, Mandela alipenda masumbwi. ''Masumbwi ni bure, Ukiwa ulingoni , umri na hadhi yako pamoja na mali yako sio muhumu,'' aliandika katika kitabu chake kuhusu maisha yake 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/06/10/130610143414_anc_439x549_ap.jpg
Mwaka 1956, alituhumiwa kwa kosa la uhaini kwa sababu ya kazi yake na ANC. Wakati wa kesi yake, alikutana na mfanyakazi wa kijamii aliyeitwa, Winnie Mandela. Ndao yake kwa Evelyn Mase iliisha baada ya wawili hao kutalakiana. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2013/06/10/130610142219_nelson_winnie_mandela_439x549_rexfeatures.jpg
Nelson na Winnie walioana mwaka 1958 lakini hawakufurahia maisha yao ya ndoa kwani wote walikuwa wakikamatwa mara kwa mara. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220150658_mandela_life_pictures_06.jpg
Kufuatia kesi ya pili ya uhaini dhidi ya Mandela, alifungwa maisha jela mwaka 1964
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220150821_mandela_life_pictures_07.jpg
Hatimaye zaidi ya miaka ishirini baada ya kufungwa jela, Mandela aliachiliwa mwaka 1990.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220153637_mandela_life_pictures_10a.jpg
Kufuatia kuachiliwa kwake, Mandela lizuru nchi nyingi na kukutana na viongozi wa dunia alipokuwa anjiandaa kuwania urais. Anaonekana hapa katika ubalozi wa Afrika Kusini mjini London ambako maandamano ya kupinga utawala wa kizungu daima yalikuwa yakifanyika.
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151330_mandela_life_pictures_11.jpg
Mashauriano makubwa yalifanyika kabla ya rais FW de Klerk kukubali au kuruhusu watu kupiga kura. Wawili hao walituzwa tuzo ya amani ya Nobbel, kwa sababu ya kumaliza ubaguzi wa rangi Afrika Kusini. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151416_mandela_life_pictures_12.jpg
Uchaguzi wa kwanaza wa kidemokrasia ulifanyika tarehe 27 mwezi Aprili m,waka 1994. Waafrika weusi walipanga foleni kupiga kura kwa mara ya kwanza. Chama cha ANC kilishinda uchaguzi huo kwa wingi wa kura na hivyo Mandela kuwa rais wa kwanza mweusi kuongoza Afrika Kusini
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151527_mandela_life_pictures_13.jpg
Mandela alitawala nchi hiyo kwa muhula mmoja pekee na mnamo mwaka 1999 akawa mmoja wa viongiozi wachache wa Afrika kuachia ngazi kwa hiari. Thabo Mbeki, alipewa jukumu la kumrithi Mandela kama rais na kiongozi wa ANC
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151611_mandela_life_pictures_14.jpg
Kando na kuwa kiongozi anayependwa zaidi duniani, pia aliweza kuonekana na mitindo ya kipekee kwa sababu ya T sheti zake nzuri nzuri. Hapa anawaluiza wandishi wa habari maoni yao kuhusu shati yake, baada ya maankuli ya mchana na muundajji wa mitindo Pierre Cardin 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151645_mandela_life_pictures_15.jpg
Pia ana mambo mawili ambayo sio kawaida kwa viongozi wa dunia kuwa nayo....mpole na mwenye kuweza hata kujicheka , hapa anakutana na mwanamfalme Prince Charles na wanamuziki wa iliyokuwa bendi ya Spice Girls
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151751_mandela_life_pictures_16.jpg
Baada ya kutalakiana na mkewe Winnie , Mandela alimuoa Graca Machel, alipokuwa anasherehekea miaka  80 mwaka 1998. Bi Machel ni mjane wa aliyekuwa rais wa Msumbiji Samora Machel. Bi Graca na Mandela walianzisha hazina ya kuwasaidia watoto wasio na uwezo mkubwa maishani 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151915_mandela_life_pictures_17.jpg
Tangu kuondoka mamlakani, mwaka 1999, bwana Mandela alikuwa mmoja wa viongozi wakuu kufanya kampeini dhidi ya ukimwi na utovu wa usalama wakati nchi yake ilipokuwa mwenyeji wa kombe la dunia mwaka 2010
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220151942_mandela_life_pictures_18.jpg
Mwaka 2004, akiwa na umri wa miaka 85, Mandela alistaafu kutoka majukumu ya umma ili kuwa na muda na faimlia yake pamoja na marafiki zake. 
http://wscdn.bbc.co.uk/worldservice/assets/images/2011/12/20/111220152058_mandela_life_pictures_19.jpg
Bwana Mandela, aliweza kujitokeza wakati wa sherehe ya kufunga michuano ya kombe la dunia mwaka huo. Hali yake ya kiafya ilikuwa mbaya na alikuwa anaomboleza kifo cha kitukuu wake aliyeuawa huku michuano hiyo ikianza.

Rais Obama alivyotikisa Msibani Afrika kusini katika kuenzi Mandela

obama+machelLicha ya kuwa ni siku ya huzuni kwa dunia nzima, hotuba ya Rais wa Marekani, Barack Obama imewagusa maelfu ya watu waliokuwa kwenye Uwanja wa FNB katika ibada ya kitaifa kumwaga Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela.
Obama aliyetumia dakika 20 katika hotuba yake iliyokuwa ikikatizwa na kelele za kumshangilia, aliwataka vijana wa Afrika na dunia nzima kuiga maisha aliyoishi Mandela kama yeye alivyojifunza mambo mengi kutoka kwa mzalendo huyo.
“Miaka 30 iliyopita nikiwa mwanafunzi, nilisoma Kitabu cha Mandela na tangu siku hiyo nilijifunza, nikajenga roho ya uthabiti. Iliamsha uwajibikaji kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu wangu… hakika Mandela amenifanya niwe hivi nilivyo leo. Michelle na mimi tumenufaika sana na Mandela,” alisema Obama na kuongeza:
“Mandela alinifanya niwe mtu ninayesimama mbele yenu leo, alichangia kunifanya kuwa kiongozi bora. Nitaendelea kuiga mfano wake,”
Katika sherehe hizo, Obama alipokewa kwa shangwe na kushangiliwa kila alipopita na kila alipozungumza tofauti na ilivyokuwa kwa Rais wa nchi hiyo, Jacob Zuma ambaye alikuwa akizomewa.
Obama alimtaja Mandela kama kiongozi anayefaa kuigwa kwani pamoja na kukaa gerezani kwa miaka 27 akipigania uhuru, hakutaka kung’ang’ania madaraka na badala yake alistaafu kwa hiari yake, tofauti na viongozi wengi wa Afrika.
“Mandela alionyesha uongozi wa vitendo na kujaribu, alikuwa ni mwanamume, binadamu wa kawaida, mume, baba na kiongozi shupavu,” alisema Obama.
Pia Obama alisema, Mandela aliachiwa huru kama mfungwa, lakini kama mwalimu ambaye alitumika kutuonyesha kuwa, ni lazima kuwaamini wenzako ili nao wakuamini.
“Kufundisha upatanisho, hakuhitaji kudharau historia mbaya ya nyuma bali ni kuikabili kwa umakini, ukweli na uhalisia wake. Mandela alibadili sheria, lakini alibadili mioyo yetu pia,” alisema.
Katika risala hiyo, Obama alimtaja Mandela kama mwanamapinduzi mkubwa wa karne ya 20 aliyeibadilisha mioyo ya watu wake, akaimarisha mapatano na maelewano kwa wazungu na weusi.
“Amezaliwa kipindi cha Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia, kijana aliyekuwa akichunga ng’ombe na kuteswa na wakubwa zake wa kikabila, lakini ameibuka na kuwa mwanamapinduzi mkuu wa karne ya 20,” alisema Obama.
Vilevile, Obama alimfananisha Mandela na Abraham Lincoln, Rais wa zamani wa Marekani kwa kuiunganisha nchi yake pale ilipokuwa inataka kuvurugika.
Rais huyo aliufanya umati katika uwanja huo ulipuke zaidi kwa furaha baada ya kuzungumza neno la Kizulu, ‘ubuntu’ linalomaanisha utu au ubinadamu ambapo alisema Mandela ameimarisha utu na ubinadamu kwa Waafrika Kusini.
“Alidumisha ‘utu’ miongoni mwetu. Utu ambao tunaweza kuupata kwa kushirikiana na kuwajali wanaotuzunguka,” alisema Rais huyo ambaye anatajwa kuwa Rais wa dunia. Obama alionyesha umahiri wake katika risala hiyo na katika sehemu ya risala hiyo alisema ni wajibu wa kila mmoja kuiga maisha aliyoishi Mandela.
“Ni lazima tujifunze kutoka kwake, kwa sababu Waafrika Kusini kwa jumla wao wameonyesha kuwa, tunaweza kubadilika.”
Obama alimtaja Mandela kama mtu asiyependa kujikweza bali aliyeshiriki kuonyesha mawazo yake na hofu na uhalisia wake hasa kwa kusema kuwa yeye si mtakatifu labda kama mtakatifu ni sawa na mwenye dhambi ambaye hachoki kujaribu. Kiongozi huyo alimalizia hotuba hiyo kwa nukuu muhimu za Mandela zinazosema kuwa, ‘Mimi ni kiongozi wa imani, mustakabali wangu, na mimi ni nahodha wa roho yangu’ na kuwataka Waafrika Kusini kuishi katika maneno hayo ya Mandela katika maisha yao.
“Hakika ilikuwa roho ya ajabu, tutamkumbuka sana. Mungu wabariki Waafrika Kusini,” alimaliza Obama. Kabla ya hotuba hiyo, Obama alifanya jambo la kihistoria kwa kupeana mikono na Rais wa Cuba, Raul Castro, kama ishara ya mapatano baada ya migogoro iliyoko baina ya nchi hizo mbili.
Kabla ya Obama kuzungumza, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon katika hotuba yake alisema kuwa, alijitoa muhanga kwa ajili ya usalama, uhuru na demokrasia ya nchi yake.
“Sherehe hizi za kumbukumbu zinadhihirisha upinde wa mvua wa taifa. Ninatumaini tutaweza kuuona upinde huo punde, kupitia mvua ya simanzi,” alisema Ki-Moon. Ki-Moon alimtaja Mandela kuwa ni kiongozi aliyejiandaa kupoteza kila kitu kwa ajili ya uhuru na demokrasia.
“Dunia imepoteza rafiki na mwalimu. Alikuwa ni zaidi ya viongozi wakubwa wa nyakati zetu; mwalimu mkuu aliyetufundisha kwa mifano,” alisema Ki-Moon.
Wakati huo huo, Mkuu wa Majeshi wa nchi hiyo, Jenerali Thanduxolo Mandela kwa niaba ya familia ya Mandela alipata nafasi ya kutoa risala yake kwa Rais huyo na alisema kuwa, familia hiyo ina bahati ya kuwa na mzazi kama Mandela.
“Utakumbukwa daima, hatuwezi kuusahau mchango wako katika familia na katika maisha ya Waafrika Kusini wote,” alisema Thanduxolo.
Baada ya Thanduxolo, walikuja wajukuu na vitukuu wa Mandela kwa niaba ya wajukuu wote, Pumla, Andile na Mbuso Mandela ambao walisema wana mengi waliyojifunza kwa babu yao ambaye walimtaja kuwa kioo cha familia na kuahidi kuwa wataishi na matendo yake.
Mandela atazikwa Jumapili.
CHANZO: MWANANCHI

Hali halisi ilivyokuwa jana katika kumbukumbu ya Nelson Mandela


ma2Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiwa na Rais Mstaafu wa Marekani Mhe George W. Bush na Mkewe Laura Bush wakiwa jukwaa la viongozi na watu mashuhuri baada ya Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela leo Desemba 10, 2013 katika uwanja wa FNB jijini Johannesburg.PICHA NA IKULU ma4Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumanne, Desemba 10, 2013, ameungana na viongozi wa mataifa mbali mbali duniani na maelfu ya wananchi wa Afrika Kusini Kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha aliyekuwa kiongozi mashuhuri wa Afrika Kusini na duniani, Mheshimiwa Nelson R Mandela.
Maelfu kwa maelfu ya wananchi wamehimili mvua kubwa iliyokuwa inanyesha kwa nguvu kwenye Uwanja wa Michezo wa FNB mjini Johannesburg kumwaga Mzee Mandela ambaye alikuwa ishara kuu ya upinzani wa siasa za ubaguzi wa rangi za makaburu wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa Mandela ambaye alifariki duniani Ijumaa iliyopita, Desemba 5, 2013, alikuwa Kamanda wa Jeshi la Ukombozi la Chama cha African National Congress la Umkhoto we Sizwe akafungwa jela kwa uhaini kwa miaka 27 na utawala wa Makaburu.
Baada ya kutoka jela mwaka Februari 1990, Mzee Mandela alichaguliwa kuwa Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini ya mwaka 1994. Lakini Mheshimiwa Mandela alitumikia kipindi kimoja tu cha miaka mitano na kukataa kutumikia kipindi cha pili.
Kiasi cha viongozi 91 kutoka sehemu duniani wamehudhuria Kumbukumbu hiyo iliyokuwa na kila aina ya mchanganyiko wa hisia – wengine wakiwa na majonzi na wengine wakicheza na kuimba kwa muda wote wa shughuli hiyo iliyochukua kiasi cha jumla ya saa tano.
Mbali na Rais Kikwete ambaye amefuatana na Mama Salma Kikwete, marais wengine mashuhuri duniani waliohudhuria Kumbukumbu hiyo ni Mheshimiwa Barack Obama wa Marekani, Mheshimiwa Francois Hollande wa Ufaransa, Waziri Mkuu wa Uingereza, Mheshimiwa David Cameroun na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN) Ban Ki Moon.
Kumbukumbu hiyo pia ilihudhuriwa na viongozi wa zamani wa Marekani wakiwemo marais watatu wa zamani wa Marekani – Mheshimiwa Jimmy Carter, Mheshimiwa Bill Clinton na Mheshimiwa George W Bush na mawaziri wakuu wawili wa zamani wa Uingereza, Mheshimiwa Tony Blair na Mheshimiwa Gordon Brown.
Rais Kikwete kesho, Jumatano, Desemba 11, 2013, ataungana na viongozi wenzake katia katika kutoa heshima za mwisho na kuuaga rasmi mwili wa Marehemu Mandela ambao utawekwa kwenye Majengo ya Urais wa Afrika Kusini ya Union Buildings mjini Pretoria.