Friday, June 1, 2012

Wachimbaji wadogo wa madini wakumbukwa na serikali, sasa kubwaboreshea mazingira


WIZARA ya Nishati na Madini imesema kwa sasa imejipanga kuwawezesha  wachimbaji wadogo nchini, hususan katika kuboresha shughuli zao.
Akizungumza na Fullshangweblog jijini Dar es Salaam jana, Naibu  Waziri wa sekta hiyo  Steven Masele alisema kwamba  mkakati huo umekuja siku chache baada ya kubaini kuwa wachimabji hao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ukosefu wa vitendea kazi.
 Alisema kwamba moja ya ongezeko la uchumi wa nchi unatokana na madini, hivyo kuna haja ya kuliangalia kundi hilo kwa lengo la kupanua pato sanjari na ajira kwa wazawa.
Aidha, alichanganua kuwa wigo wa wizara hiyo umekuwa kwa asilimia 3.3 tofauti na awali ambapo ulikuwa asilimia 0.6.
"Wachimbaji wadogo wamekuwa wakiendesha shughuli zao katika wakati mgumu sana, hasa kwa kukosa vitendea kazi vya kuaminika  jambo ambalo limekuwa likisababisha  wengi wao kufariki wakiwa migodini"alisema Masere.
Naibu huyo, alivitaja baadhi ya vifaa ambavyo wachimbaji hao wanavyohitaji kuwa ni pamoja na mashine za kuingiza na kutolea hewa chafu, ya kuingia na kutoka wakati wakiwa migodini.  

No comments:

Post a Comment