RORYA KWETU

Pata habari moto moto kila siku, kwa Mawasiliano zaidi piga Simu Na. 0755 856991/ 0712 992434 Email:-theonestinajuma@yahoo.com/rorya.09@gmail.com

Monday, April 30, 2012

Yaliopita si ndwele, lakini.... Ati wanabeza lugha yetu iliotuunganisha na kuwa kitu kimoja miaka nenda rudi!

Na Theonestina Juma, Uganda
KUTOKANA na baadhi ya viongozi wa nchini Uganda kudai kuwa hawajisikii vizuri Kiswahili kutumika katika mazungumzo ya Ushirikiano wa Jumiya ya Afrika Mashariki katika mkutano uliotangulia juzi iliwalazimu kukaa kimya baada ya viongozi kutoka Tanzania kukitumia lugha hiyo kuanzia mwanzo hadi mwisho wa majadiliano.
Hayo yalibainika Oktoba 24, mwaka 2011 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa mpira wa Malaba wilaya ya Rakai nchini Uganda, uliohudhuriwa na Naibu wa Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Shirikisho la Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) nchini humo, Bw. Eriya Kategaya ambaye ndiye alikuwa mgeni rasmi, pamoja na ujumbe kutoka Tanzania ulioongozwa na Naibu Waziri wa (EAC) wa Tanzania, Bw. Abdallah Sadallah.
Katika Mkutano huo, ambao mtu wa kwanza kuzunguza na wananchi katike eneo hilo alikuwa ni Mkuu wa Mkoa Kagera, Kanali Fabian Massawe ambaye katika utambulisho wake alilazimika kujibu mapigo kwa kutumia lugha ya Kiswahili bila kuchang’anya na lugha ya kiingereza katika mkutano wake wote.
Akizungumza katika mkutano huo, Kanali Massawe alisema lugha ni kitu muhimu na ili waweze kushirikiana ni lazima itafutwe lugha moja itakayotumiwa katika mawasiliano na kuelewana tofauti na hivi sasa, ambapo kunajitokeza mkanganyiko.
“Lugha ni kitu muhimu na ya msingi sana katika mawasiliano, na ili tuweze tushirikiane, itafutwe lugha moja ya mawasiliano hata kama ni Acholi, Kiganda, kihaya …..lakini mambo ya kutumia makalimani ni kuonesha udhaifu wa ushirikiano wetu”alisema.
Alisema iwapo itapatikana lugha yoyote moja itakayokubalika kutumika jumuiya hiyo wananchi pamoja na viongozi wao hawana budi kukijifunza kwa bidii, kwa ajili ya maendeleo yao.
“Hebu angalieni Wazungu mfano kama Marekani wanatumia lugha gani kuu ya mawasiliano… wao wamechagua lugha moja ya mawasiliano na ndiyo maana wameweza kupiga hatua”aliongeza.
Hata hivyo, aliwaomba viongozi wanchi hizo kutumia vyombo vya habari vya kijamii vilivyoko mikoani katika kuelimisha wanachi juu ya shirikisho hilo kwani vyombo hivyo navyo vina nguvu katika jamii inayowazunguka.
Naye Naibu Waziri Mkuu wa nchini humo, Bw. Kategaya akizungumzia historia ya Kiswahili nchini Uganda alisema wananchi wengi wao wanajua kuwa Kiswahili ni lugha ya majambazi wanaopora mali za wananchi na askari wanaoitumia kwa kutoa amri hali iliowajengea woga wananchi na kukichukia.
Alisema licha ya lugha ya Kiswahili kuchukuliwa kwa mtizamo huo, lakini katika kiserikali ni lugha ya mawasiliano na ni lugha kuu inayotumiwa na watu wengi wa Afrika Mashariki.
Alisema pamoja na hali hiyo, kupitia wizara yake na ya elimu nchini humo, unafanya mpango ambapo hadi kufika mwakani lugha hiyo itaanza kufundishwa kuanzia elimu ya msingi lengo likiwa ni kutaka kukiendeleza ili wananchi wa nchini humo waweze kukielewa katika mawasiliano.
Katika kikao kilichofanyika juzi nchini humo katika ukumbi wa Juuko’s wilayani Rakai baadhi ya viongozi wa nchini humo, wakioongozwa na Mkurugenzi (CHO) wa wilaya hiyo,Nkato James  walionesha wazi kukibeza lugha ya Kiswahili ambayo ni lugha ya saba duniani kwa madai kuwa hawajisikii vizuri kukizungumza, ambapo walitaka lugha ya kiingereza na kiganda ndizo zitumike.
Katika mkutano huo wa siku mbili ulilenga  kujadili masuala ya ushirikiano wa jumuiya ya Afrika Mashariki, mafanikio, fursa na changamoto zinazozikabili nchi wananchama kati ya Tanzania na Uganda kwa upande wa maeneo ya mipakani.
Mwisho.


Posted by www.theonestinaj.blogspot.com at 3:48:00 PM
Email ThisBlogThis!Share to XShare to FacebookShare to Pinterest

No comments:

Post a Comment

Newer Post Older Post Home
Subscribe to: Post Comments (Atom)

YALIYOMO

  • ▼  2012 (389)
    • ▼  April (33)
      • "Padri apigwa butwaa kumaliza miaka sita bila kuen...
      • ushirikina mpaka lini?
      • Mwili wa Kanumba unafanyiwa uchunguzi leo
      • kilichomuua Kanumba ni hiki hapa
      • Misa ya mazishi ya Kanumba yanaendelea katika ukum...
      • Jinsi wasanii wenzake walivyokuwa katika msiba huo...
      • RPC Malawi atimuliwa kazi na Rais Banda
      • Haijawahi tokea maziko ya Kanumba labda ya Mwal.Ny...
      • BREKING NEWZZZZZZZ LULU KIZIMBANI CHINI YA ULINZI...
      • ELIZABETH MICHAEL A.K.A LULU KIZIMBANI
      • USAFI UKIWA UMEPAMBA MOTO KATIKA MANISPAA YA BUKO...
      • BILIONI 11 KUJENGA SOKO LA KISASA BUKOBA
      • "KUPATA KIWANJA BUKOBA KWA SASA NI HELA YAKO TU."
      • Katibu Tawala wa Biharamulo ang'olewa jino na JWTZ
      • Bilioni 120 zatumika kuboresha migomba nchini
      • Mawaziri wanne wa JK wadaiwa kuachia ngazi
      • Sijaamini kama nimetoka hai katika ajali hii.
      • Matukio katika picha.
      • "Babu tulikupenda sana, kwa kheri"
      • Upumzike kwa amani Mzee wetu Mpendwa.
      • Elizabeth 'Lulu' apandishwa tena kizimbani, sasa a...
      • Wajumbe wa mkutano Mkuu KCU 1990 Ltd wapigwa mbumb...
      • Tudumishe mila zetu.
      • Ati anamsafirisha Simba kwenye baiskeli!
      • Leo ni siku yangu ya kuzaliwa, asante Mungu kwa ku...
      • Hapo vipi?
      • Mmoja wa wajumbe wa mkutano mkuu wa mezania wa C...
      • 'Hatuondoki, hata kama mkiwaleta kikosi cha FFU'-W...
      • Amani na maendeleo... Kagera, Kagera... Amani na M...
      • Mambo yote ni sawa ilimradi tuvuke salama.
      • Uwepo wa Mungu unapoonekana hivi.......Mugana.
      • Kwa wenzetu wa nchi jirani ya Uganda usalama uko hivi
      • Yaliopita si ndwele, lakini.... Ati wanabeza lugha...
    • ►  May (69)
    • ►  June (120)
    • ►  July (39)
    • ►  August (22)
    • ►  September (15)
    • ►  October (33)
    • ►  November (14)
    • ►  December (44)
  • ►  2013 (118)
    • ►  January (23)
    • ►  February (3)
    • ►  March (2)
    • ►  May (10)
    • ►  June (7)
    • ►  July (22)
    • ►  August (15)
    • ►  September (24)
    • ►  October (3)
    • ►  December (9)
  • ►  2014 (75)
    • ►  January (13)
    • ►  February (7)
    • ►  March (22)
    • ►  April (4)
    • ►  May (5)
    • ►  June (1)
    • ►  July (2)
    • ►  August (6)
    • ►  October (10)
    • ►  November (3)
    • ►  December (2)
  • ►  2015 (13)
    • ►  April (1)
    • ►  May (2)
    • ►  July (10)

KUHUSU MIMI

www.theonestinaj.blogspot.com
BUKOBA, KAGERA, Tanzania
Theonestina Juma, ninaishi Bukoba Kagera Tanzania.Napenda watu wanaojituma kwa kufanya kazi.Sipendi wanaobeza shughuli za wengine.
View my complete profile
Powered By Blogger
Theonestina Juma (Rorya kwetu. Watermark theme. Powered by Blogger.