Sunday, September 8, 2013

Operesheni Kimbunga yaanza rasmi ya kuwarejesha wahamaji haramu makwao, ni agizo la Rais Kikwete



Na Theonestina Juma, KAGERA
OPERESHENI kimbunga ya kuwarejesha wahamiaji
haramu makwao katika Mikoa ya Geita, Kagera na Kigoma imeanza rasmi ambapo ndani ya siku mbili tu, wahamiaji hamu 1851 na ng'ombe 10763 wamekamatwa.
Hayo yamebainishwa jana (leo) na  Mkuu wa Operesheni nchini,Simon Sirro ambaye pia ni Mkuu Msaidizi wa operesheni kmbunga katika mkutano na Waandishi wa habari kuhusiana na operesheni ulioanza rasmi Septemba 6, mwaka huu kufuatia agizo la Rais
Jakaya Kikwete alilotoa akiwa ziarani Mkoani Kagera mwishoni mwa mwezi Julai mwaka huu.
Kamanda Sirro alisema katika Operesheni hiyo iliopewa
jina la "Operesheni Kimbunga" kwa siku mbili tu, timu ya vyombo vya usalama wanaoshiki katika zoezi hilo, wamekamata wahamiaji haramu 1851, ng'ombe 1763, silaha za moto saba ikiwemo short gun moja pamoja
na vifaa mbali mbali vya jeshi ikiwemo na sare za JWTZ. 


 Kanal Fabian Massawe akieleza mbele ya waandishi wa habari kuanza kwa operesheni ya kuondoa wahamiaji haramu na wanaomiliki silaha kinyume na sheria.
  Mkuu wa Mkoa Kagera Kanal Massawe akiwa na Mkuu wa operesheni nchini na Mkuu wa operesheno Kimbunga Kamanda Simon Sirro amewataka wananchi wote kutoa ushirikiano katika zoezi zima ambalo amesema halina mwisho mpaka hapo watakaporidhika.                             
                                                     baadhi ya maafisa wa jeshi la polisi mkoa wa Kagera


 
Alisema katika mkoa wa  Kigoma wamekamatwa wahamiaji haramu 855, short gun moja, gobole moja na ng'ombe 200, Mkoa wa Geita wahamiaji haramu 246
wamepatikana, gobole tatu na ng'ombe 240, sare ya jeshi moja na kibuyu cha maji cha JWTZ moja.
Halikadhalika Mkoa wa Kagera Wahamiaji 750
wamekamatwa, short gun moja, gobole sita, ng'ombe 1,323, ambapo ng'ombe 200 walikamatwa ndani ya pori la akiba la Moyovosi Kigoma na wengine 200 wamekamatwa katika pori la akiba la Burigi mkoani Kagera.
Alisema ng'ombe 1,123 wamekamatwa wilaya za Karagwe na Kyerwa na 240 kutoka maeneo mbali mbali mkoani Geita.
Alisema miongoni hao wahamiaji haramu 750 waliokamatwa mkoani Kagera, 26 wamekatwa katika Manispaa ya Bukoba.
Kamanda Sirro alisema katika zoezi hilo, wahamiaji hao wanawapakia kwenye malori na kuwapeleka hadi mipakani wa Tanzania nan chi husika na kuwakabidhi kwa viongozi wan chi husika.
“Katika harakati za kutekeleza zoezi hili, suala la haki za binadamu tunazingatia sana, kwani wahamiaji haramu tunawaondoa kwa upole na utaratibu unaotakiwa”alisema
Alisema katika utekelezaji wa zoezi hilo, ametoa onyo kali kwa mtu yeyote ambaye watawarushia risasi maofisa wao, hawatakuwa na mchezo nao, tuko tayari kupambana na yeyote atakayejaribu kuwarushia risasi"alisema.
“Huu si wakati wa kuchezeana kwa kurushiwa risasi, kwani muda waliopewa kusalimisha silaha ziliisha kama yeye ni raia mwema muda huu hatakiwi kuwa na silaha yoyote kinyume cha sharia, kama  mtu anasilaha heri aitelekeze huko huko porini”alisisitiza.
Aidha aliwataka wananchi wenye haki wasihofu lolote waendelee na shughuli zao za maendeleo.
Kwa upande wa Mkuu wa mkoa wa  Kagera, Kanali Fabian Massawe amewaka vyombo vinavyoendesha operesheni kuwa makini katika zoezi hilo kwa kuzingatia haki za binadamu.
Alisema wanatakiwa kuhakikisha wahamiaji haramu hao wanaondoka na vitu vyao na wananchi wasikubali kuwahifadhia mali zao.
"Kuna taarifa kuwa kuna baadhi ya wahamiaji haramu, wanawapatia wananchi kuwahifadhia mali zao, tunataka waondoke navyo na kama wana wauzia iwe katika maandishi mtu yeyote atakayebainika kuhifadhi vifaa vya wahamiaji haramu watakamatwa na kushtakiwa kwa kuhujumu nchi"alisema.
Aidha Kanali Massawe alisema katika zoezi hilo
halitawakumba wale wahamiaji haramu wa kike waliolewa na Watanzania wanatakiwa kwenda idara ya uhamiaji ili kuweza kupewa hati maalum na baadaye kuhalalishiwa uraia wake.
"Katika utekelezaji wa zoezi hili kuna malalamiko kuwa wanawake ambao ni wahamiaji haramu wanarudishwa,
huku baadhi yao wakiwa na watoto watatu hadi sita, hatuko kwa ajili ya kutenganisha ndoa za watu, wale walioondoka bila kujua sharia wanatakiwa kurudi kama walivyoondoka"alisema.
Alisema lengo la serikali si kwa ajili ya kuachanisha familia za watu na wala hawatamfukuza mtu kwa vile amemwoa mhamiaji hamu katika utekelezaji wa agizo la Rais Kikwete.
Alisema kabla ya kuanza kwa zoezi hili jumla ya wahamiaji haramu 11,061 waliondoka  mkoani Kagera, silaha 65 zilisalimishwa SMG zikiwa tatu,Short gun 10 na magobore 52.
 Alisema pamoja na idadi hiyo kuondoka kwa  hiari  mkoa ulitazamia kuondoka kwa wahamiaji haramu 52,000 -53,000 hivyo idadi ya wahamiaji haramu bado ni kubwa.
Amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa timu ya operesheni kwa kuwataja wahamiaji haramu
waliko ili sharia iweze kuchukua mkondo wake.

Juali 26, mwaka huu Rais Kikwete akiwa wilayani Biharamulo alisema operesheni hiyo ambayo itaendeshwa katika mikoa hiyo itakuwa ni ya aina yake ambayo haijahi kutokea katika nchi hii. 


No comments:

Post a Comment