Wednesday, September 26, 2012

Niko Tayari kushiriki mazishi ya Kadinali Rugambwa hapo Oktoba 6, 2012

Yap, niko tayari kwa siku hiyo muhimu katika historia ya maisha yangu, ikizingatiwa kuwa wakati Kadinali Rugambwa akifariki dunia nilikuwa kidato cha tatu, bado kinda sasa mazishi yake rasmi mimi bonge la mama.


Changia kanisa kwa kununua sare zao rasmi ili kufanisha sherehe hizo.Hiki kitenge nilichojifunga ni moja ya aina ya sare itakayotumika siku hiyo ya Oktoba 6, mwaka huu, siku ambayo mwili wa Kadinali Rugwambwa utahamishwa kutoka katika Parokia ya Kashozi alikozikwa kwa muda na kisha kupumzishwa katika nyumba yake ya milele katika kanisa Kuu la Jimbo la Bukoba.Siku hiyo maelfu ya wageni wanatarajiwa kufurika katika Manispaa ya Bukoba.

No comments:

Post a Comment